Daktari Ataja Ugonjwa Unao Msumbua Mbosso


Daktari Ataja Ugonjwa Unao Msumbua Mbosso
 
Baada ya video za mwanamuziki Mbosso kusambaa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonyesha akiwa hospitali amelazwa. Msanii huyo ameweka wazi kuwa alikuwa akisumbuliwa na tatizo la Umeme wa Moyo kwa muda mrefu lakini kwa sasa amepona kabisa.

"Kwa sasa kijana wenu nimepona kabisa ugonjwa wa moyo uliokuwa unanisumbua kwa kipindi cha miaka yote na jana jioni nimeruhusiwa kuendelea na mapumziko nyumbani na baada ya wiki 1 niweze kuendelea na majukumu yangu ya kila siku,” ameeleza Mbosso kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Ameeleza kuwa juzi Februari 11, 2025 ilikuwa siku ya hofu kwake, mashabiki na kwa familia yake. Lakini alifanikiwa kupatiwa matibabu ndani ya saa moja na sasa amepona kabisa.
Post a Comment (0)
Previous Post Next Post